MRADI WA KUPUNGUZA AJALI ZA VIJANA KUANZIA UMRI WA MIAKA 15-29


FAST AND MOBILE EDUCATION (F.M.E) FOR BODABODA AND SPECIAL GROUPS AT KISARAWE.
BY Gwemela Michael.
Blogger.

UTANGULIZI.

Kutokana na takwimu zilizopo za wizara ya afya zilizotolewa na vyombo vya habari zinaonyesha kuwa kuna uwepo mkubwa wa vifo wa vijana wenye umri kati ya miaka 15-29 kwa njia ya ajali, ikifuatiwa na kujiua Kutokana na changamoto mbalimbali za maisha.
·        Kwa uwepo wa vifo hivyo, sisi afrotalent, vijana ambao tupo kwenye rika hilo tumeamua kuingilia kati na kupunguza kama ikiwezekana kuzuia vifo hivyo.
·        Kwa kuanza na wilaya ya kisarawe, tunatamani kufanya yaliyo orodheshwa hapo chini.

JINA LA MRADI: FAST AND MOBILE EDUCATION (F.M.E)
F.M.E, ni mradi mahsusi Kwa makundi maalumu kama yatima na wasiojiweza, pia unawahusu watu wote wanaokosa elimu ya msingi kuhusiana na changamoto zao za kila siku, kama vile bodaboda na vibarua.
Huu mradi ki ufupi unawahusu watu wote wenye uhitaji wa elimu ya kiuchumi na kijasiliamalia haswa kutoka kwenye hali dhaifu na mbaya waliomo, na kujikwamua kiuchumi.
ENEO.
            Wilaya ya Kisarawe.
MISINGI ELEKEZI.
A.    KUJIDHATITI.
Kujitoa kwa dhati kwenye mradi huu pasipo na wasiwasi na kuhamasisha kwa uelewa wetu wote.
B.     HESHIMA.
Kuheshimu kila program ambayo tutaiweka katika vitendo kwa kuhakikisha uwepo wa uhalisia wa program husika.
C.     HUDUMA YETU.
Kusimamia na kutekeleza mradi huu wa (FAST AND MOBILE EDUCATION) Kwa Makundi maalumu pamoja na makundi yasiyo maalumu ila yako kwenye hatari ya kudhurika na mazingira kama bodaboda.





WAHUSIKA.

 SPECIAL GROUPS.

Image result for special groupImage result for special groups
copied: from ctc-ck.com                      ctc-ck.com
2.     Mobile na fast education kisarawe itawahusu watoto wote wanaoishi kwenye mazingira magumu na pia Makundi mengine yote special kama wakina mama wajane, vilema,vipofu,ulemavu wa ngozi(albino).
3.     WATU MASHUHURI NA MAARUFU.
Watu maarufu kama Mh. Mkuu wa wilaya, Jokate Mwegelo na watu wengine wote walio maarufu kama inspiration icon kwenye maisha yetu ya kila siku pasipo na uwepo wao, yamkini elimu kwa ushuhuda itakosekana na pia itapendeza kama watu hao mashuhuri watatoa ushuhuda unaoendana moja kwa moja na maisha magumu wanayoyapitia watu hawa.
4.     SERIKALI.
Wahusika wa ngazi hii ni serikali kwa ujumla ambapo kwa mradi huu umerengwa moja kwa moja kwenye ngazi ya wilaya ya kisarawe, hivyo uwepo wa shughuli hii katika ngazi ya wilaya,pia shughuli hii itafanyika katika ngazi ya wilaya.
Na hawa ndio watakaokuwa wamiliki wa mradi huu Kutokana na uhalisia wa mradi wenyewe, yaani utafanyika ndani ya wilaya ya kisarawe na pili utawahusu viongozi wa kisarawe na mwisho utapewa nguvu na halmashauri/manispaa ya kisarawe ili kuleta madhara chanya.
5.     AFROTALENT.
Hawa ni wanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma ambao wanabeba ndoto zilizokufa za jamii nyingine ikiwemo ile ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu huku wakikosa elimu,chakula,mavazi na hata pa kulala na hivyo kujikuta wakilala maeneo hatarishi kama kwenye misingi ya madaraja na wakati mwingine kufariki kwa kupitiwa na mvua, pia hawa vijana hutoa elimu ya ujasilia mali ambapo wanasema kuwa  ‘‘Elimu ya shuleni kwa mtu aliyekwisha ikosa sio dhambi kwake  kiasi cha kujilaumu milele bali anaweza kujifunza elimu msingi na kujua yeye ni nani na kisha kukuza talanta yake hiyo njema’’.
Afrotalent inaundwa na MICHAEL NKANWA na GWEMELA CONRAD MICHAEL ikiwa na member takribani 40 ambao wamekuwa kama volunteer katika shughuli mbalimbali za afrotalent na hivyo kupeleka Mbele baadhi ya shughulina kufanya zifike kwa kiwango kile ambacho Tulikuwa tumekusudia.
6.     WANACNCHI.
Wananchi wa kisarawe wote ni walengwa  wa mradi huu kwa unalenga kuingia kwenye jamii yao moja kwa moja ili iweze kuwa na fursa ya kuwapatia Makundi maalumu ya watu ili kuwafungua na kuwajengea hatima yao kwa kuwashawishi washiriki kwenye baadhi ya programu ambazo zitakazokuwa zikifanyika

UTEKELEZAJI WA MRADI.
Mradi na utekelezwaji wake utakuwa kwenye programu mbalimbali katika jamii ya Kisarawe kama ifuatavyo;

PROGRAMU.
Mobile na fast EDU ndani ya kisarawe itakuwa na majikumu ya kuendesha programu mbalimbali ili kuhakikisha adhma yake ya kuwafungua Makundi maalumu ya wasiojiweza ili kufanikisha malengo yao ya kila siku ili Kujenga jamii imara ambapo kila mmoja wetu anaifurahia. Zifuatazo ni programu mbalimbali ambazo zitafanyika kwa wakati mradi huu.
1.     MOBILE AND FAST EDU.
Itakuwa ni programu yetu ya kwanza ambapo ina lengo ya kuwafikia walengwa takribani 10000. Programu hii ina lengo la kuwafikia watu wote walioko kwenye mkusanyiko wa Kundi maalumu ambao hawakupata elimu ya kusoma na kuhesabu.
Kwa kutumia mfumo wetu wa “I teach you and you teach me” programu itawafikia wahusika tajwa kwa haraka na kuwezesha watu husika kuelewa kusoma na kufanya hesabu ndogo ndogo ambapo itawasaidia kwenye kujijenga kiuchumi.
-         Kwa kipengele hiki cha mobile and fast edu, watoaji wa elimu watakuwa ni
a)     Traffics, hapa mkuu wa matraffic atazungumzia usalama na sheria za barabarani
b)    Viongozi wakubwa wa serikali, watatoa mwongozo wa kisheria wa wapi watu hawa wanapaswa kufuatilia haki zao za kimsingi kisheria ili kuwezesha ndoto zao.
c)     Wanafunzi wote waliokwishafanikiwa ambao asili yao ni wilayani kisarawe watapata nafasi ya kuongea ili waweze kuja nyumbani kufanya motivational talks na kuwa hamasisha watoto,vijana,wakina mama,na wazee na wale wote waliokata tamaa ya maisha
d)    Mwisho kwenye program hii ni afrotalent ambao hawa watatoa elimu juu ya namna ya kuishi katika mazingira magumu na kutoa elimu ya ujasiliamali ili kuepuka ajali za barabarani na Kujenga ajira nje ya bodaboda.


2.     SAFE BIKE FOR SAFE KISARAWE.
              Image result for ajali za pikipiki
picha:copied from mwananchi.co.tz
-         Hii itakuwa program ya pili ambapo kila kijana atashiriki haswa kwa vijana wanaoshiriki uendeshaji wa bodaboda na hivyo kutoa impact kwa jamii husika ya waendesha bodaboda ili kuwezesha usafiri wa bodaboda ni salama na pia kuminiwa na wateja wake.
-         Takwimu u zinaoenesha vifo vingi vya vijana vinatokana na ajali, na chanzo cha pili cha vifo hivyo ni kujiua . Ambapo kwa upande wa ajali ni ajali nyingi zinazohusishwa moja kwa moja na zile za vyombo vya moto hasa barabarani.
-         Hivyo kwenye program hii tutatoa elimu kuhusu namna nzuri ya kutumia vyombo vya moto kabla,wakati na baada ya kuendesha bodaboda kwa kuwatembelea kwenye vituo vyao vya kazi.
-         Mfano, kama pikipiki imewekewa mafuta na dereva anahisi mafuta yamekwisha, sisi tutampa funzo hili… FUNZO; mafuta hasa ya petrol yanaweza kulevya hivyo kwa yeyote anaeendelea kunusa kama ishara ya kujua ujazo wa mafuta hapo huwa anakosea kwani anachokifanya ni kuvuta kilevi pasipo kujua na hivyo kushambulia mfumo wake kati wa kufikiri na hivyo kumfanya awe maamuzi hafifu hivyo hata kwenye eneo la barabarani anaweza kutafsiri alama ya kutopita kwenye njia ya wapitamiguu kama ni eneo lake. ….NINI TUFANYE? Sisi kama bodaboda tunapaswa kujifunza kujua mafuta yakiwa yamekwisha kwa kuangalia kwenye dashboard.
-         Mfano wa pili ni uwezekano wa pikipiki au gari kulipuka wakati wa kujaza mafuta huku vyombo hivyo vikiwa vimewashwa. Hivyo jinsi ya kufanya ni kuzima gari au pikipiki na hivyo kuzuia ajali.

3.  MY SCHOOL MY CARRIER.
Image result for my school
copied from: amazon.co.uk
Kwenye program hii hapa kisarawe itafanyika kwenye shule zote za secondary na zile za msingi ili kuhamasisha ufaulu wa darasani huku ikiwa na lengo kuwafanya wanafunzi wenyewe kuwa na uwezo binafsi wa kujiendeleza hata kama watashindwa kujifunza na elimu ya juu ya upili kiasi kwamba wataweza kujijenga kiuchumi na kuachana na mawazo ya kushiriki katika udereva wa bodaboda na kuhakikisha wanakuwa na uelewa wa moja kwa moja kuhusiana na madhara ya barabara.
-         mambo yatakayofanyika moja kwa moja ni kutoa jtatu jioni moja na jmosi moja kwa ajili ya elimu kwa vitendo kwa kila wiki na hivyo kuwapa fursa vijana wa kidato cha tatu na kidato cha nne kuhudhuria ili  waweze kukutana na elimu hiyo muhimu ili iwe msaada kwao hapo baadae.
-         Kwa upande wa wanafunzi kufanya vizuri kwenye mitihani yao watatakiwa wa adopt hii program ya “I read, you read, we read”. Ambapo kwenye program hii kila darasa litasimamiwa na mwalimu wa darasa na huku wanafunzi watahusika na eneo lingine lote la programu hii litafanywa na wanafunzi wenyewe.
PROGRAM hii itahusisha muundo wa mpira wa miguu ili kurahisisha uwasilishaji wa wazo kuu.
                    I.            Kocha.
                 II.            Refa.
               III.            Vibendera.
              IV.            Wachezaji.
Msimamo wa programu.
“kila mmoja ana jukumu la kushiriki kikamilifu kwenye programu hii ili iweze kuleta matokeo chanya”
UFAFANUZI WA PROGRAMU HII.
Ø Makocha.
Hili litakuwa Kundi la wanafunzi wenye uwezo wa juu kidogo au zaidi ya wenzao kwa kila somo. Hii itahusisha kila somo mwanafunzi tofauti hata kama mwanafunzi mmoja anaweza masomo yote peke yake.
Ø Refa.
Hili litakuwa ni Kundi la wanafunzi ambao watakuwa na kazi ya Kukusanya maswali yanayohusiana na uhitaji wa wanafunzi wa darasa husika, na kuyapeleka kwa  makocha kwa ajili ya kuatatuliwa, hivyo kila kabla ya kipindi maswali yanajibiwa darasani na kuwapa fursa wanafunzi kujua majibu ya maswali yao. Na kama yatashindwa kwa makocha(wanafunzi wenye uwezo) hapo ndipo yatapelekwa kwa mwalimu wa somo husika.
Ø Vibendera.
Linesmens au vibendera huyu atakuwa ni mwalimu special ambaye naye atakuwa na jukumu la kutatua matatizo madogomadogo ya program kama upatikanaji wa chalk na pia upatikanaji wa majibu ya maswali ya vijana hawa. Pia mwalimu huyu ndie atakaye kuwa na nafasi ya kutolea ufafanuzi wa program hii ili kuhakikisha kila darasa lina program hii na hivyo kufanya uwezekano wa kuendelea kwa program hiyo hivyo kuwezesha uendeshaji kwa ujumla wa program hii.
Ø WACHEZAJI.
Darasa zima kutoa makocha na marefa, hili litakuwa Kundi la wanafunzi lilogawanyika katika safu nne;
                               I.            Mlinda mlango.
Itakuwa ni safu ya kukinga na kuondoa hatari zote zitakazokuwa zikielekea kwenye program hii. Wanafunzi hawa wanapaswa kuwa wenye busara, japo sio mara zote lakini mara nyingi ni wale viongozi wa dini zote, waislamu na wakristo na dini nyingine.
                             II.            Safu ya ulinzi.
Hawa watakuwa wanafunzi ambao watakuwa na kazi ya kuibua maswali na njia au suluhu ambazo hazikueleweka na darasa kwa ujumla,( hivyo aina ya wanafunzi hawa inatakiwa iwe ile ya wanafunzi ambao ni wadadisi), wayarudishe maswali na suluhu hizo tena kwenye mdaharo na kuwezesha kurudiwa ili kila mmoja aelewe.
                          III.            Safu ya kati.
Hili litakuwa Kundi ambalo linahusika na Kukusanya maswali ya darasani pamoja na mitihani ya nyuma na kuigawanya darasani aidha kwa kuandika ubaoni au kwa kugawanya karatasi na kuhakikisha utunzaji wa maswali mengine kwa ajili ya wakati husika hapo baadae.
                          IV.            Safu ya ushambuliaji.
Mwisho kutakuwa na Kundi la wanafunzi ambao hawa watakuwa ni wenye kusimamia na kuangazia sheria za shule na pia hawa watakuwa na kazi ya kuwashirikisha wanafunzi wa shule jirani ili kujipima uwezo binafsi.
Hawa pia watakuwa wana kazi ya kutoa vipaumbele vya kufanya wakati wa program hii, vinavyohusiana na muda sahihi kwa kila shughuli.
NB; KILA KIPENGELE KILICHOPO CHENYE KUHUSISHA WANAFUNZI KINAWEZA KUUNGANISHWA NA UONGOZI WA SHULE WA WANAFUNZI.
MAPENDEKEZO.
Sisi kama afrotalent tunapendekeza “kuwa na sheria ndogo juu ya Udereva wa bodaboda itakayozingatia umri wa madereva, sheria za barabarani,kuvaa vifaa  vya usalama kati ya dereva na abiria”
 kama utapenda kazi hii nifuate inbox kwangu kwa email hii gwemelaconrad@gmail.com

Post a Comment

THANK YOU FOR A COMMENT!

Previous Post Next Post